Siku ya Alhamisi, Rais wa Urusi Vladimir Putin alitangaza kwamba kuanguka kwa Umoja wa Kisovieti ndiko kulikosababisha migogoro katika nchi ambazo zilikuwa miongoni mwa jamhuri zake, ikiwa ni pamoja na Ukraine.
"Inatosha kuangalia kile kinachotokea sasa kati ya Urusi na Ukraine na kile kinachotokea katika mipaka ya nchi zingine ndani ya Jumuiya ya Madola Huru," Putin alisema wakati wa mkutano wa televisheni na wakuu wa huduma za kijasusi wa nchi za zamani za Soviet. Yote haya, bila shaka, ni matokeo ya kuanguka kwa Muungano wa Sovieti.”
Putin aliendelea: “Tumegeuka kuwa nchi tofauti kabisa. Kile kilichojengwa kwa zaidi ya miaka 1000 kimepotea kwa kiasi kikubwa,” akasema, akibainisha kwamba Warusi milioni 25 katika nchi mpya zilizokuwa huru walijikuta ghafula wakiwa wametengwa na Urusi, sehemu ya kile alichokiita “msiba mkubwa wa kibinadamu.”
Putin pia alielezea kwa mara ya kwanza jinsi yeye binafsi alivyoathiriwa na nyakati ngumu za kiuchumi zilizofuata kuanguka kwa Soviet, wakati Urusi ilikumbwa na mfumuko wa bei.
"Wakati mwingine (nililazimika kufanya kazi mbili na kuendesha teksi," rais wa Urusi alisema. Haipendezi kuzungumza juu ya hili lakini, kwa bahati mbaya, ilitokea