Zaidi ya watu mia moja na hamsini waliuawa mjini Seoul wakati wa sherehe za Halloween
Rais wa Korea Kusini Yoon Sok-yul Jumapili alitangaza maombolezo ya kitaifa baada ya mkanyagano uliotokea wakati wa sherehe za Halloween na kusema ni bahati mbaya sana kuona maafa kama hayo yakitokea katikati mwa Seoul.
Takriban watu 149 waliuawa katika mkanyagano uliotokea baada ya idadi kubwa ya watu kuanguka kwenye uchochoro mwembamba wakati wa sherehe huko Seoul Jumamosi usiku, maafisa wa dharura walisema.
Choi Sung-beom, mkuu wa Kituo cha Zimamoto cha Yongsan, aliambia mkutano wa habari kutoka eneo la tukio kwamba wengine 150 walijeruhiwa katika ajali hiyo katika wilaya ya Itaewon ya Seoul.
Maafisa walisema wengi wa waliojeruhiwa wako katika hali mbaya na wanapokea matibabu.
Hii ni sherehe ya kwanza ya Halloween katika kipindi cha miaka mitatu na inakuja baada ya nchi kuondoa vizuizi vya kupambana na coronavirus na sheria za umbali wa kijamii. Wengi wa washiriki katika sherehe walivaa vinyago na kuvaa mavazi ya Halloween.